Na Henry Bernard Mwakifuna, Ifakara-Kilombero
MBINU ya Shamba Darasa inatarajiwa kusaidia kupunguza tatizo la Uhaba wa Maafisa Ugani Vijijini.
Juliana Njombo,Mwezeshaji wa Shamba Darasa katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero amewaambia Washiriki wa Mafunzo kwa Wataalamu wa Kilimo kuhusu Dhana ya Shamba Darasa kuwa Mkulima aliyeshiriki ipasavyo katika mafunzo ya Shamba Darasa anakuwa Mtaalamu na anauwezo wa kusaidia Wakulima Wengine.
Amesema Kuwa pindi mkulima anapowezeshwa na mwezeshaji wa Mafunzo ya Shamba Darasa anakuwa Mtaalamu baada ya Kuhitimu naye anawafundisha wenzake na kutanua wigo kwa wakulima wengine katika kila kipindi cha msimu wa Kilimo na hivyo kusaidia kupunguza tatizo la Maafisa Ugani katika baadhi ya Vijiji.
Lengo kuu la Mafunzo hayo ya Siku Nne yanayoshirikisha Maafisa Ugani wa Vijiji Saba,Wataalamu kutoka Ofisi ya Kilimo Wilaya ya Kilombero Wawili,wawezeshaji Wawili na watu wa Kada nyingine Jumla yao 15 ni washiriki kuweza kupata ujuzi wa kuanzisha na kuendesha shamba Darasa katika Maeneo husika.
Mafunzo hayo yanayoendeshwa na Wawezeshaji kutoka Idara ya Kilimo ya Halmashauri ya Kilombero inasimamiwa na Shirika lisilo la Kiserikali linalojihushisha na Mazingira katika Bonde la Kilombero (KIVEDO) chini ya Ufadhili Serikali ya Ujerumani kupitia Wizara ya Uchumi na Maendeleo kupitia Plan International.
No comments:
Post a Comment