Na Ferdinand Nachenga
Jana nilipata bahati ya kutembelea kivuko cha Mto Kilombero maarufu kama kivukoni mida ya saa kumi na mbili jioni. Nikakaa kwenye pub ya upande wa Ifakara japo ilikua inanuka maana kuna choo kisichosafichwa kwa muda mrefu karibu na hiyo pub.
Hapakua na watu,nikaagiza kinywaji kisha nikapanda juu na kuanza kuangalia mandhari ya bonde la Kilombero. Nilichoshuhudia ni jinsi gani kilimo na ufugaji vilivyoathiri mto kilombero. Sijawahi kuona maji ya mto huu kukauka kiasi kile,nadhani ulimaji karibu kabisa na mto pamoja na ufugaji inabidi vipigwe vita sana ili kunusuru mto huu na bonde kwa ujumla.
Pantoni lilikua linaendelea na shughuri zake japo wanasema mwisho saa kumi na mbili jioni. cha ajabu ni kwamba pantoni haina taa inatumia taa za magari yanayopakiwa humo dah nilisikitika sana huku niki...kumbuka kilichotokea miaka kadhaa iliyopita.
Kufika saa mbili hivi nikashuka chini na kuona mlinzi anazuia watu wasiingie maana muda umeisha lakini kama una 500 unaruhusiwa na pikipiki ni 2000 bila kutoa risiti. Nami nikajifanya nataka kuvuka lakini jamaa alisema bila 500 nisubiri kesho na mia mbili yangu.
Wenye pesa walienda na wengi masikini walikwama hasa wakina mama. Nilipouliza kwa nini wanafanya hivyo nikaambiwa wao wakale wapi? kwa hiyo zile zote ni zao. Niliumia sana lakini huo ndio uozo wa uongozi wa wilaya yetu. yani hata taa ya pantoni hawawezi kununua? Ajali ikitokea nani alaumiwe? nani atafidia wahanga?kwa gharama ipi? ..we need to act now guys....
No comments:
Post a Comment