Henry Bernard Mwakifuna, Ifakara-Kilombero.
Makundi matano kati ya 17 yaliyokuwa yakishiriki Ngoma za Utamaduni yametolewa na Majaji kufuatia kupata alama chache.
Baadhi ya vigezo vilivyotumika katika Tamasha hilo ni pamoja na Ujumbe, Mpangilio wa Sauti, uchangamfu wa Wachezaji, Sare na Matumizi ya Muda.
Mratibu Pacha wa Tamasha hilo Joseph Mlango amevitaja Vikundi vilivyotoka ni Segere cha Machipi, Tupendane cha Michenga, Kasi Mpya cha Mlabani, Libeneke cha Lipangalala na Kinyago cha Viwanja Sitini vyote Wilayani Kilombero.
vikundi vilivyobaki ni Gunia Tupu Halisimami cha Mlabani,Ya kale Dhahabu cha Miomboni-Mofu, Lumumba cha Mangwale,Toma Toma cha Kikwawila, Twitange cha Mangwale, Maji Marefu cha Katindiuka na Saga na Kukoboa cha kibaoni.
vingine Vilivyobaki ni Sega Dansi cha Mlabani, Fuka Fuka, Lizombe cha Machipi na Iragua Group kikundi pekee kutoka Wilayani Ulanga.
Tamasha hilo lililoandaliwa na Tumaini Development and Counseling Trust (TUDECO) wakishirikiana na Makutano Club Ifakara lilianza Septemba ya Pili na Fainali yake inatarajiwa kufanyika Septemba ya 30 Mwaka huu.
No comments:
Post a Comment